• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

MAKAMU WA RAIS ALETA NEEMA SAME SEKONDARI

Posted on: March 21st, 2024

Ujio wa Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt.Philip Mpango kwenye Wilaya ya Same umeleta neema kwa Shule ya Sekondari Same kuchimbiwa visima vya maji baada ya shule hiyo kukosa maji ya uhakika kwa muda mrefu.

Dkt.Mpango alifika kwenye shule ya Sekondari Same kuotesha mti kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani na siku ya upandaji miti kitaifa ambapo pia alipata ,muda wa kuongea na wanafunzi wa shule hiyo kongwe yenye wanafunzi wa kidato cha tano na sita wapatao 950 ambayo ilianzishwa mwaka 1952.

Wanafunzi hao walitumia fursa hiyo vizuri ambapo waliwasilisha kilio chao cha ukosefu wa maji ya uhakika jambo linalosababisha wakati mwingine wapeane zamu za kuoga.

Akitoa neno la shukrani kwa Makamu wa Rais kufika na kuotesha mti shuleni hapo, Mwanafunzi wa kidato cha sita Joshua Mwakijangala   alimuomba Makamu wa Rais kusaidia upatikanaji wa maji shuleni hapo.

“Mheshimiwa Makamu wa Rais tumefurahi sana wewe kufika hapa shuleni kwetu,hapa shuleni tuna changamoto ya upatikanaji wa maji tunaomba utusaidie tupate maji ya uhakika” aliomba Mwanafunzi huyo.

Aidha mwanafunzi huyo aliomba pia Serikali kusaidia ukarabati wa mabweni au ujenzi wa mabweni mapya ili kuweza kukidhi uhitaji wa mabweni pia tunaomba kupatiwa walimu wa Sayansi.

“Tunashukuru Serikali imekarabati mabweni mawili makubwa na pia imetujengea bweni moja jipya lakini bado tuna uhitaji wa nyongeza ya mabweni” alisema Mwanafunzi Joshua.

Akijibu maombi hayo Makamu wa Rais Mheshimiwa Mpango alimwagiza Waziri wa maji Juma Aweso aliyekuwepo kwenye msafara huo kuhakikisha kuwa visima vinachimbwa shuleni hapo ambapo Waziri Aweso aliahidi utaratibu wa kuchimba kisima utaanza Machi 22,2024.

Kuhusu nyongeza ya mabweni Mheshimiwa Makamu wa Rais alisema serikali itaongeza mabweni ambapo pia aliagiza katika ajira mpya za walimu shule hiyo ipatiwe walimu wa Sayansi.

Siku ya Misitu Duniani na uoteshaji miti kitaifa huazimishwa Machi 21 ya kila mwaka na mwaka huu imeffanyika kitaifa wilayani Same,Kilimanjaro ikiwa na kaulimbiu isemayo “Misitu na Ubunifu”

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WACHIMBA MADINI SAME WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    May 19, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAOMBA WIZARA YA KILIMO KUIPATAIA MICHE YA PARACHICHI

    May 01, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.