• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

ANDIKO LA SAME UTALII FESTIVAL LAKABIDHIWA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Posted on: September 26th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda J. Mgeni,amekabidhi andiko la uendeshaji wa Tamasha la Same Utalii Festival (SUF) kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bw.Nkoba Mabula

Andiko hilo lina lengo la kutangaza na kukuza Utalii kwenye Wilaya ya Same ili kuweza kuinua Uchumi wa Wilaya ya Same.

Mheshimiwa Mgeni alisema utalii si tu fursa ya kiuchumi, bali pia njia ya kuboresha maisha ya wananchi na kuhifadhi mazingira na kufurahia rasilimali zilizopo hapa nchini.

“Wilaya yetu ya Same imezungukwa na hifadhi mbalimbali na vivutio vingine vya asili kama maporomoko ya maji na Mipango"alisema

 Alisema Tamasha la Same Utalii Festival ambalo liliana rasmi mwaka huu litakuwa endelevu na litafanyika kila mwaka.

Aliongeza kuwa tamasha hilo ni jukwaa muhimu la kuhamasisha jamii kuhusu faida za uhifadhi na jinsi unavyoweza kuchangia katika ustawi wa kiuchumi.

Mgeni alitoa shukrani kwa Rais kwa kuendelea kutekeleza sera za maendeleo ya utalii, akieleza kuwa Wilaya ya Same ina vivutio vingi ambavyo havijatangazwa.

"Tumeona ongezeko la wageni, na kampuni tano tayari zimejitokeza kusafirisha watalii baada ya kuona muitikio wa watu kwenye tamasha la kwanza,” aliongeza, akionyesha matumaini makubwa kuhusu maendeleo ya utalii katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nkoba Mabula, alisisitiza umuhimu wa kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo wilayani humo.

"Nimekuja kuona baadhi ya vivutio vyetu,nchi hii imebarikiwa, lakini tunahitaji orodha ya vivutio ili tuweze kufanya kazi zaidi ya kuvitangaza,” alisema.

Mabula alitaja umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na wananchi katika matumizi ya rasilimali za misitu, mashamba, na hifadhi ili kuongeza mapato.

Aidha, aliupongeza uongozi wa wilaya kwa kufanikisha tamasha la utalii, lakini alisisitiza umuhimu wa kuwa na vituo vya taarifa za utalii kila Wilaya.

Aliongeza kuwa, Wizara iko tayari kutoa ushirikiano kufanikisha tamasha hilo, akiamini litakuwa fursa ya kuimarisha utamaduni wa Wapare na kuwahamasisha wawekezaji kuzingatia mila na desturi za eneo. “Tunataka fedha zinazopatikana kutokana na utalii zibaki hapa Same,” alisisitiza.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WACHIMBA MADINI SAME WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    May 19, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAOMBA WIZARA YA KILIMO KUIPATAIA MICHE YA PARACHICHI

    May 01, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.